Na mwandishi wetu
MWENYEKITI wa Chama Cha Makini Taifa, Coaster Kibonde,amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa hotuba yake iliyojaa ukoma na weledi aliyoitoa mbele ya wazee wa Jiji la Dar es Salaam.Kibonde amesema hotuba imeonyesha ujasiri mkubwa na ni ya mfano kwani imeweka sura ya nchi kwamba ina kiongozi shupavu na jasiri mwenye dhamira ya kulinda amani na utulivu wa Taifa.
Akizungumza na mwandishi kwa mahojiano maalum amesema kwamba ameonyesha sauti ya mamlaka ya kwamba Tanzania inaendeshwa kwa mujibu wa Sheria haiwezi kuingiliwa na nchi nyingine yoyote.
Aidha,Kibonde alisema kwamba ni muhimu kwa wananchi kuheshimu maagizo ya mamlaka zilizopo kwa manufaa ya Taifa.
"Hakuna kiongozi anayetamani wananchi wake wapate shida .Kila kiongozi mwenye busara hutaka kuona watu wake wakiishi kwa furaha,amani, upendo na utulivu",alisema
Pia amewataka vijana nchini kuendelea kudumisha amani na kutii Sheria hasa kipindi hiki kinapoelekea tarehe 9 Desemba.
Sanjari na hayo,Amesema kwamba viongozi wa dini wana nafasi kubwa ya kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kulinda na kutetea amani,hivyo vijana wanatakiwa kusikiliza maongozi ya kirohi yanayojenga jamii tulivu.
