MHE. GHATI CHOMETE AIPONGEZA KAMPUNI YA FREGOM LTD KUIBUKA KINARA ULIPAJI KODI MKOANI MARA 2025.

 


MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara Mhe.Ghati Zephania Chomete ameipongeza Kampuni ya uchimbaji na ununuzi wa dhahabu "FREGOM LTD" kwa kuibuka kuwa kinara kwa ulipaji wa kodi kundi la "Makampuni ya Madini" Mkoani Mara kwa Mwaka 2025.

Kampuni ya FREGOM LTD chini ya Mkurugenzi wake Ndg.Fredy Masiaga yenye Makao Makuu Mjini Musoma, Mkoani Mara imepokea hati ya shukrani na pongezi kutoka kwa Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara kwa kuibuka kuwa kinara wa ulipaji kodi bora kwa Mwaka 2025 kundi la "Makampuni ya Madini" Mkoani Mara.

Akiongea Soko Kuu la Dhahabu Mkoani Mara hapo Jana tarehe 24 Desemba, 2025 Mhe.Ghati Chomete (Mb) aliwaeleza wachimbaji na wanunuzi wa dhahabu kuwa sekta ya madini itafanikiwa endapo watu wote wataendelea kulinda amani na utulivu wa nchi yetu.

Post a Comment

Previous Post Next Post